Tuesday, 15 September 2015

KATIBA YA SACCOS


WACHAGA WOTE SACCOS (WAWOSA) LTD

 About Wachanga wote saving and credits cooperative society (WAWOSA).

Kilianzishwa rasmi tarehe 01/09/2015 kwa juhudi za mwasisi wake ambaye ni ndugu August August Kessy (Sundaypesa), chini ya uongozi thabiti wa Maafisa ushirika akiwemo ndugu Emanuel Kessy na ushauri mzuri wa walezi wa chama Josephina Kessy, Deogratius Lyimo, Rose Mallya pamoja na John Chacky.

Chama hiki cha SACCOS kilianzishwa kwa madhumuni ya kusaidiana katika shida na raha kama vile:- Msiba, Harusi na Send - off party.

Unaweza kujiunga popote pale ulipo ndani ya Tanzania au hata nje ya Tanzania kwa kuwasiliana nasi kwa namba zetu na e-mail yetu ili kuwa mwanachama wetu.


KATIBA YA SACCOS
(a).     Ili kuwa mwanachama wa SACCOS lazima uwe na umri wa miaka (18) na
kuendelea mwenye akili timamu na lazima uwe wa kabila la Wachaga wa Mkoa wa Kilimanjaro.

(b).     Gharama iliyo pendekezwa kwa kumchangia mwanachama mwenye mahitaji
husika hapo juu  ni bei ya gazeti au vocha yani uwe msiba, harusi au send - off party ni Sh elfu moja 1,000/= tu  bila kujali tukio husika. Hivyo basi gharama hiyo itamsaidia mwanachama kumudu kuchangia  awe mwenye kipato cha juu, kipato cha kati na mwenye kipato cha chini.


(c ).     Mwanachama atakaye funga ndoa kwa upande wa mwanaume tunamchangia
kiasi cha sh elfu   moja 1000/=.

(e).      Mwanachama atakaye olewa kwa upande wa mwanamke tunamchangia kiasi
cha elfu moja 1,000/=

(f).      Gharama ya kujiunga kwa mwanachama ni sh. elfu tano tu 5,000/=

(g).     Gharama ya ada ya mwanachama kwa mwezi ni sh. elfu moja tu 1,000/=
unaweza kulipia ada   ya miezi sita yani sh. elfu sita 6,000/= au kulipa pia ada ya mwaka yani sh. elfu kumi na mbili   tu 12,000/= .

(h).      Mwanachama aliyepatwa na ataizo husika anatakiwa kuwasiliana na      
mwenyekiti wa   SACCOS na mwenyekiti atawataarifu wanachama wote wa WAWOSA kwenye simu zao



(i).        Pindi mwanachama anapopata taarifa hasa ya msiba kwenye simu yake.
anatakiwa awasilishe mchango wake ndani ya saa ishirini na nne (24). Hiyo itasaidia maandalizi muhimu  ukizingatia msiba hauchukui muda mrefu sana

(j).        Taarifa kuhusu harusi na send - off party mwanachama anapopata taarifa
             anatakiwa   awasilishe mchango wake ndani ya wiki moja.

(k).      Mwanachama asiyechangia wenzake ndani ya matukio matatu yaliyotokea
            bila sababu   maalumu atakuwa amejitoa mwenyewe ndani ya chama.

(l).        Mwanachama atachangia tatizo husika tu pindi linapotokea iwe msiba, harusi
  au send-off  party.

(m).      Kama hakuna tatizo ndani ya mwezi mzima mwanachama hatohusika na
            mchango wowote ule zaidi ya ada yake ya mwezi.

(n).       Michango yote pamoja na ada ya mwanachama itumwe kupitia namba ya 
M-PESA 0756  150093 na TIGO - PESA 0654 238488 jina litakalotokea kwenye simu yako  hakikisha ni AUGUST  A. KESSY   Mwenyekiti wa chama.

(o)        Kauli mbiu yetu ya chama "CHANGIA NA WEWE UCHANGIWE" au
  "UMOJA NI  NGUVU NA UTENGANO NI UDHAIFU."

(p).       Kwa maoni, maswali au ushauri tuandikie hapo chini kwenye sehemu ya
           maoni au tupigie  kwenye namba zetu hapo juu.


             Ahsanteni sana.
















No comments:

Post a Comment